TyDiQA1.0

The Typologically Different Question Answering Dataset

Predictions

Scores

Hussein Mkiety

The Typologically Different Question Answering Dataset

Mkiety ni mtoto wa mwisho wa familia ya watoto watatu wa Ramadhani na Zainabu Mkieti. Alizaliwa tarehe 27 Oktoba, 1985 katika kijiji cha Lusanga, Muheza, Tanga.Alipata elimu ya msingi katika shule ya Lusanga na baadaye kujiunga na sekondari ya Kwabutu alikosoma hadi kidato ya tatu, akaacha shule kutokana na matatizo ya kifamilia. Mwaka 2003 baada ya kuona maisha hayaendi, aliamua kuhamia Kiwalani, Dar es Salaam, kuungana na mama yake ambaye alikuwa mjasiriamali mdogo.Baada ya kufika Dar, alipelekwa kujifunza masuala ya ufundi magari kwenye gereji moja ambako alidumu wiki mbili na baadaye kupelekwa kwenye ufundi mafriji ambako alijifunza kwa wiki tatu, nako hakudumu baada ya kuona kipato hafifu. Kuanzia hapo akaamua kuhamia kwenye biashara ndogo na hasa ilikuwa kuuza magazeti hukohuko Kiwalani.[3]